• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

Mradi wa Kilimo cha Korosho

Start Date: 2019-01-01
End Date: 2030-12-31

HALMASHAURI YA WILAYA YA MANYONI

TAARIFA YA KILIMO CHA KOROSHO

  1. UTANGULIZI: 

Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni ni miongoni mwa Halmashauri 7 za Mkoa wa Singida yenye hali ya hewa inayofaa kwa kilimo cha korosho kutokana na utafiti uliofanyika na watafiti wa kilimo kutoka Taasisi ya Utafiti wa mazao ya kilimo Naliendele kwa kushirikiana na watafiti wa mazao ya Kilimo Kanda ya Kati.

Baada ya kupitia tafiti hizi Uongozi wa Halmashauri uliona uanzishe zao korosho kuwa zao Mkakati, ili liweze kuchochea kwa kasi kubwa ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na wa Wilaya hata Mkoa kwa ujumla.

Ilibainika wazi kuwa zao hili linaweza kuwa zao kubwa la Biashara katika Wilaya Manyoni na Mkoa wa Singida, linaweza kuvutia uwekezaji wa Viwanda katika Mkoa huu.

Uongozi  Halmashauri ya Wilaya Manyoni uliamua kuanzisha kilimo cha pamoja (block farming) lenye ukubwa wa takribani ekari 12,000 ambapo wamiliki wa mashamba ni wakulima na Halmashauri inasimama kama msimamizi mkuu wa hatua zote za kilimo bora, ambapo shamba hili pia linatumika kama shamba la mfano kwa  wakulima wengine pia ambao wako nje ya eneo la mradi huu wa shamba la pamoja (Block Farming)

  1. KILIMO CHA KOROSHO MSIMU 2017/2018

Katika msimu wa kilimo 2017 Halmashuri ya wilaya ya Manyoni ililenga kulima ekari 1,382 ambapo ilipokea pembejeo za zao la korosho kutoka Bodi ya korosho kwa lengo la kuzalisha miche bora ya korosho na kuisambaza kwa wakulima. Idadi ya miche halisi iliyozalishwa na kusambazwa kwa wakulima ni  109,752.

Aidha, kutokana na mwamko wa wakulima Halmashauri ya Wilaya ilipokea miche 9,867 kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

Miche iliyozalishwa ilisambazwa kwa wakulima katika maeneo mbali mbali ndani ya halmashauri ambapo katika Shamba la pamoja (Block farming) ilipelekwa miche 37,000 na miche mingine 82,119 ilipelekwa katika vijiji vingine ambavyo vipo katika halmashauri ya wilaya ya Manyoni.

 

 

  1. SABABU ZA KUCHAGUA KOROSHO KUWA ZAO MKAKATI MANYONI

Sababu kuu tatu zilizofanya Uongozi wa Halmashauri kuchagua zao la Korosho kuchagua zao la Korosho kuwa zao Mkakati la Wilaya ni hizi zifuatazo:-

  1. Zao hili lilikuwa tayari limefanyiwa utafiti wa kina na Taasisi ya Serikali ya Kilimo ya Naliendele na kutoa tarifa yake kuwa zao hili linastawi kwa uhakika katika Halmashauri ya Wilaya Manyoni na Mkoa wa Singida katika maeneo mengi.
  2. Tayari ilishabainishwa kuwa zao la korosho linaweza kuwa zao la kudumu la biashara litakalowapatia wananchi kipato na kuwa na uhakika wa chakula.  Hii ni kutokana na Halmashauri  ya Wilaya ya Manyoni kwa kipindi kirefu haikuwa na zao la kudumu la biashara wananchi waliuza mazao ya chakula ili kupata kipato. Hivyo zao la korosho llimewekewa mkakati madhubuti wa kuliendeleza zao hili kwani litakuwa  mkombozi wa wakulima kwa kipato na usalama wa chakula.
  3. Katika maeneo tofauti ya Halmashauri ya Wilaya Manyoni wananchi wengi huko nyuma walishaonesha mwitikio wa kupanda korosho japo kwa kiasi kidogo mno lakini katika maeneo tofauto. Wamnanchi walitumia mikorosho hiyo kama miti ya vivuli kwa sababu ilistawi vizuri kuliko miti mingine waliyowahi kupanda katika maeneo yao. Mikorosho hiyo hutumiwa hata kwenye maeneo wanayokaa kwa ajili ya vikao mbalimbali kwa matumizi ya kujikinga jua.

Kutokana na sababu hizo Uongozi uliamua kutenga maeneo ambayo yataweza kuanzishwa shamba la Mfano ambalo litalimwa kama shamba la pamoja (Block farming) ili liwe shamba kuwafundishia wananchi na pia kiwe kichocheo kikubwa cha uchumi wa Halmashauri kuweka soko la korosho katika eneo moja kubwa na chanzo kikuu cha ushuru wa Halmashauri.

 

 

Mwanzo wa usafishaji wa mashamba katika shamba la pamoja la kilimo cha korosho

  1. SABABU ZA KUAMUA KUWA NA SHAMBA LA PAMOJA

Tunamkumbuka sana Baba wa Taifa hayati Mwl Julius Kambarage Nyerere ambaye alitumia muda wake mwingi kuanzisha mashamba ya Ushirika katika maeneo mbalimbali Tanania miaka ya 1970. Baba wa Taifa alikuwa na maono makubwa na alikuwa na uchú wa kuona Tanzania inapaa kwenda kwenye uchumi mkubwa, yawezekana wakati ule kizazi kilichokuwa na nguvu ya kushika uchumi hakikumuelewa vizuri.

Zipo faida nyingi za kuwa na shamba la pamoja, tunaweza kubainisha wazi faida nyingi za kuwa na mradi huu ikiwa ni pamoja na kuanzisha uchumi wa pamoja wenye nguvu kubwa ambayo hawezi kuianzisha mtu mmoja kwa haraka kiasi ambacho kitawanufaisha wananchi wengi kwa muda mfupi, kudhibiti kutokea kwa majangwa katika mikoa ya kanda ya kati,  kuanzisha kilimo cha pamoja cha zao la korosho na  kuanzisha shamba kubwa la kuzalisha mbegu bora za korosho kwa ajili ya kuzisambaza kwa wakulima wa Mkoa wa Singida na Mikoa mingine.

Aidha, kilimo hiki cha pamoja kina manufaa mengine makubwa ikwa ni pamoja na;

  • Kurahishisha upatikanaji wa huduma za ugani
  • Upatikanaji wa pembejeo
  • Udhibiti wa pamoja wa visumbufu (magonjwa na wadudu)
  • Udhibiti wa ubora wa korosho 
  • Upatikanaji wa  soko

Ili shamba hili liweze kukua kwa haraka, Serikali iliamua kutoa eneo bure kwa wananchi wote wenye kukubaliana na lengo la Halmashauri kufanya zao la Korosho kuwa zao Mkakati. Ili wananchi hao waoneshe utayari wao wa kulima Korosho walihitajika kutoa Sh 20,000 kwa ekari moja kwenye Kitongoji husika kwa ajili ya maendeleo ya kitongoji hicho ambacho kilitunza ardí hii ya Serikali.

 

  1. FAIDA ZA MRADI HUU WA KILIMO CHA PAMOJA
  • Chanzo kikuu cha malighafi za viwanda vya kusindika korosho
  • Kuwepo kwa shamba hili la pamoja kutaongeza idadi ya wakulima  wanaoshiriki katika uzalishaji wa zao la korosho
  • Ongezeko la kipato kwa  wakulima wa  eneo husika 
  • Kuongezeka kwa mapato ya Halmashauri katika ushuru na kodi za biashara mbalimbali zitokanazo na ongezeko la uchumi katika sekta mtambuka zinazoendana na zao hili.
  • Hali ya maisha kuboreka ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba bora, ongezeko la kusomesha watoto na kumudu  huduma za afya.
  • Kuongezeka kwa uhakika wa chakula katika kaya  kwani wataepuka kuuza mazao ya chakula.
  • Kupatikana kwa ajira kwa wananchi mbalimbali.
  • Ongezeko la matumizi ya zana na pembejeo  za kisasa za kilimo.
  1. UTEKELEZAJI KATIKA MSIMU 2018/2019 

Katika msimu huu mwitikio uliongezeka na wananchi waliojitokeza kuunga mkono kilimo cha zao mkakati la Korosho waiongezeka, Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kwa kushirikiana na wadau wa kilimo cha korosho ililenga kupanda korosho katika shamba la pamoja kufikia ekari 7,000.

                                                                       

Mandalizi ya ufyekaji na kuchoma 2018/2019

Kulikuwa na mahitaji ya mbegu ni  kilo 5,000 kwa ajili ya kupanda shamba la masgati ekari 7,000  na kinangali ekari 5000 na pia kwa wakulima waliopo nje ya shamba la pamoja (block farming) vijiji na vitongoji 41  takribani ekari 13,000.

Pia Halmashauri iliomba sulfa ya unga  kilo 3,000 na viatilifu vinginevya maji lita 5,000

 

  1. UFUNGUZI WA TAWI LA BODI YA KOROSHO TANZANIA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MANYONI

Bodi ya korosho Tanzania imefungua tawi lake hapa Manyoni ambalo litahudumia  Mikoa ya Singida, Tabora, Kigoma na Katavi. Tunaishukuru serikali ya awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa MHESHMIWA RAIS Dr. John Pombe Magufuli  kwa kutuchagua sisi Manyoni kuwa makao makuu ya Tawi hilo kwa ajili ya kuhudumia mikoa tajwa hapo juu.

Aidha, Ufunguzi wa  tawi hili umeongeza mwitikio wa wakulima kujiunga na kilimo hiki pamoja na kuhudumia pia mikorosho ya zamani.

  1. KAZI ZINAZOTARAJIWA KUFANYIKA

A: Ukuzaji zao la Korosho

  • Usajili wa wakulima wa korosho waliopo katika Halmashauri
  • Kuhamasisha wakulima wajiunge na kilimo cha korosho
  • Kuendelea kutoa huduma za ugani kwa wakulima ikiwa ni pamoja na matumizi sahihi ya viuatilifu kwa kushirikiana na Bodi ya Korosho
  • Kuendelea na kazi ya kusafisha na kugawa mashamba kwa wakulima
  • Kuzalisha miche bora ya korosho kwa ili kuhakikisha kila msimu wa upandaji unapofikia wakulima wote waliohamasishwa wanapanda korosho.

  B: Kuboresha miundombinu kimkakati

  • Usajili wa wakulima wa korosho waliopo katika Halmashauri.
  • Kuhamasisha wakulima wajiunge na kilimo cha korosho.
  • Kusimamia kwa karibu katika uboreshaji wa pembejeo, Wataalam (maafisa ugani), Maghala, Masoko, Utafiti, Urasimishaji wa Mashamba, Huduma mbalimbali za kukuza uchumi kama barabara, umeme, maji, zahanati, usafirishaji na elimu ya mapokeo ya kilimo cha korosho kwa wananchi.
  1. GHARAMA MISIMU YA 2017/2018 NA 2018/2019

Katika misimu ya 2017/2018 na 2018/2019, Jumla ya Sh 608,113,907 kati ya Sh 619,627,000 zilitumika katika maandalizi ya mashamba na kuhakikisha eneo lililokuwa tayari katika shamba la pamoja linapandwa korosho.

Kati ya Sh 619,627,000 wakulima (wananchi) walichangia sh 582,656,800 na Halmashauri iliongezea sh 36,970,000 kuhakikisha maandalizi ya shamba yanakamilika katika maandalizi ya misimu yote ya 2017/2018 na 2018/2019.

 

  • KAZI ZITAKAZOFANYIKA KWA MSIMU 2019/2020
  • Kutafuta maeneo mapya kwa kilimo cha korosho
  • Kufungua akaunti ya mradi
  • Kutoa matangazo kwa waombaji
  • Kuandaa michoro ya shamba
  • Kuandaa mabrudoza kwa ajili ya kusafisha shamba
  • Kusafisha shamba
  • Kuandaa mbegu bora
  • Kugawa maeneo baada ya kusafishwa
  • Kusimamia upandaji wa miche ya korosho
  • VIKAO
  • Vilifanyika vikao mbalimbali vya kisheria tangu mwaka 2016 wakati wa kuanzisha mradi mkakati wa zao hili la Korosho. Vikao hivi vilianzishwa Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya Manyoni baada ya kubaini tafiti ya zao hili zilizofanyika na kuona kuwa eneo la Masigati lilichguliwa na Chuo cha utafiti wa kililo cha Naliendele kuwa liendelezwe kwa uanzishwaji wa zao hili.
  • VIKAO NGAZI YA KATA MKWESE

Tarehe 18/4/2019 kamati tendaji ya Halmashauri ilikutana na kamati ya maendeleo ya Kata ya Mkwese (WDC) kwa ajili ya kuwasilisha maombi ya eneo la kulima korosho kwenye vitongoji vya Stendi, Kinangali, Tambukareli,Miyomboni, Majengo na Mbuyuni.

  Maazimio ya kikao cha tarehe 18/4/2019.

  • Kamati ya maendeleo ya kata ya Mkwese (WDC) imepokea kilimo cha zao la korosho kwa asilimia 100 na wao wataenda kuwaelimisha wananchi umuhimu na faida ya zao hili.
  • Fedha ya maombi ya tsh 20,000/=kwa kila ekari itarejeshwa kwenye vitongoji husika kulingana na ukubwa wa maeneo yao kwa ajili ya kuchochea maendeleo kwenye kitongoji na kata kwa ujumla.
  • Watu wote watakaokutwa wamefyeka au wanalima mazao mengine  na wao watajumuishwa kwenye mradi wa kilimo cha korosho.
  • Eneo la ekari 500 litatengwa kwa ajili ya wananchi wanaopenda kulima korosho na watapewa bure ila kwa sharti la kulima korosho na siyo kuuza.
  • Kitongoji cha Stendi, kuna watu waligawiwa  maeneo mwaka 2018 kwa ajili ya kulima korosho ila hadi tarehe ya kikao cha leo siyo zaidi ya watu 10 wamefyeka na eneo lipo la kutosha. Masharti ilikuwa hadi mwezi Oktoba, 2018 kama mtu atakuwa hajafyeka atakuwa amepoteza sifa na eneo atapewa mtu mwingine
  • KIKAO CHA WAKULIMA NA KAMATI TENDAJI YA HALMASHAURI

Tahere 11/05/2019 palifanyika mkutano kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Manyoni kwa kuwashirikisha wadau wote wa korosho.Wakulima walitoa maoni yao ili kufanikisha zao la korosho kwenye Halmashauri yetu ya Manyoni na pia kwa waombaji wapya walipewa maelekezo kwa ajili ya msimu wa 2019/2020 na moja ya mambo muhimu tuliyokubaliana na wakulima ni

  • Kila muombaji aombe kulingana na uwezo wake.Ekari ni kuanzia 5 hadi 20 kwa watu binafsi ila kwa makampuni,mashirika,taasisi au vikundi ni kuanzia ekari 5 hadi 50.
  • Maombi kwa msimu wa 2019/2020 yalifunguliwa tarehe 11/5/2019   na mwisho wa maombi ilikuwa  tarehe 31/05/2019.
  • Mwisho wa kutuma fedha ya kusafisha shamba ni tarehe 30/9/2019
  1. GHARAMA ZA MAOMBI NA USAFISHAJI

Kuna aina mbili za gharama ambazo ni gharama za kuomba shamba na gharama ya kusafisha shamba.

  • Gharama ya kuomba shamba kwa kila ekari ni Tshs. 20,000 tu. Fedha hizi zitarejeshwa kwenye Kitongoji husika kulingana na eneo lililopatikana kama tulivyokubaliana kwenye kikao cha tarehe 18/4/2019.
  • Gharama ya kusafisha.Muombaji atatoa Tshs. 150,000 kwa kila ekari ili asafishiwe eneo lake. Mkulima atasafishiwa kwa mashine hivyo yeye atakuja kupanda mwezi Novemba, 2019.Aidha mkulima ambaye atashindwa kusafisha eneo lake hadi tarehe 30/9/2019 atakuwa amepoteza sifa na eneo lake atapewa mtu mwingine na fedha ya maombi haitarejeshwa.
  • Pia tumeruhusu mtu binafsi kusafisha eneo lake yeye mwenyewe kama hana uwezo wa kutoa tsh 150,000/=isipokuwa atatakiwa kukamilisha usafishaji tarehe 30/9/2019  na endapo atashindwa atapewa mtu mwingine.
  1. HALI HALISI KWA MSIMU WA 2019/2020
  • Hadi tarehe 6/6/2019 jumla ya Wananchi 341  walijitokeza na kuomba ekari 4500  kwa ajili ya msimu wa 2019/2020.Hivyo jumla ya ekari 5000 zitasafishwa na kupandwa kwa msimu wa 2019/2020 kwa wananchi wa Mkwese kugawiwa ekari 500 bure na ekari 4500 zimeombwa na Watu,taasisi,makampuni,Jeshi na vikundi mbalimbali.Vitongoji vitakavyohusika  kwa msimu 2019/2020 ni  Tambukareli,Stendi,Mbuyuni na Kinangali.
  • Kazi ya usafishaji imeanza tarehe 18/6/2019 na inatarajiwa kukamilika septemba 2019. kwa sasa barabara ya mpaka yenye zaidi ya kilometa 2 imefunguliwa na kazi inaendelea.Brudozza 2 zipo  shambani na nyingine mbili zinatarajiwa kuanza kazi tarehe 5/7/2019.1
  • Jumla ya ekari 1238 zimeshalipiwa fedha ya  usafishaji ya tsh 150,000/=.Zoezi ni endelevu.
  • Fedha za maombi.Jumla ya tsh milioni 30,000,000/=(million thelathini) zimewekwa kwenye kitongoji cha stendi kwenye akaunti namba  50710011085 inayojulikana kwa jina la KITONGOJI STENDI.Maelekezo yameshatolewa kwenye kitongoji cha Tambukareli kifungue akaunti  ili nacho kiwekewe fedha.Mchakato wa ufunguaji akaunti unaendelea.

             

  • HITIMISHO
  • Kutokana  hamasa na mwitikio uliopo kwa wananchi, halmashauri, serikali ngazi ya Wilaya na Mkoa katika kuendeleza kilimo cha zao hili tunatarajia kuzalisha korosho kwa wingi na kuwa chanzo kikuu cha kipato na uhakika wa chakula kwa wakulima, Halmashauri na Taifa kwa ujumla. Pia chanzo cha malighafi kwa ajili ya maendeleo ya viwanda vya korosho katika Halmashauri yetu ya Manyoni na maeneo mengine. Aidha, kutokana na uchanga wetu katika kilimo hiki tunaomba serikali na mamlaka nyingine husika kutusaidia hasa katika upatikanaji wa pembejeo (mbegu bora na viuatilifu vya kudhibiti magonjwa na wadudu) vipatikane katika bei ambayo wakulima wetu ambao ni wapya wataimudu.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2020 January 15, 2021
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa kidato cha pili (FTNA) 2020 January 15, 2021
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Darasa la nne (SFNA) 2020 MANYONI January 15, 2021
  • JINSI YA KUPATA SHAMBA LA KOROSHO MSIMU WA 2019/2020 May 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Waziri Lukuvi apiga marufuku viongozi wa Vijiji na Vitongoji kuuza ardhi

    January 11, 2021
  • TRC NA MIKAKATI YA UREJESHO WA HALI ZA MAISHA KATIKA MRADI WA SGR MANYONI

    December 23, 2020
  • Baraza lahimizwa kuweka kipaumbele katika Viwanda na uzalishaji wa Malighafi

    December 18, 2020
  • Naibu waziri wa kartiba na Sheria Mh. Geofrey Mizengo Pinda atembelea Manyoni.

    December 14, 2020
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni

    Sanduku la Posta: S.L.P 60, Manyoni

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 712 028027

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.