• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

"TUENDELEE KUTOA ELIMU JUU YA KODI KWA WANANCHI WETU"

Imewekwa Mtandaoni mnamo: June 21st, 2025


Haya yamesemwa na Mhe. Dkt. Vincent Mashinji Mkuu wa Wilaya ya Manyoni tarehe 21 Juni 2025 kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri wa Kodi Wilaya ya Manyoni kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Manyoni.

"Tuendelee kukutana na wananchi kwa maana ya wafanyabiashara wetu kuwapa Elimu juu ya ulipaji wa Kodi hizi, Tuwe na vikao nao mara kwa mara kwa makundi tofauti tofauti ili Elimu ya ulipaji wa Kodi hizi iwafikie wananchi wote"


Naye Ndg Frank Sigareti Meneja TRA Wilaya amesema

Wafanyabiashara wengi wamezoea kulipa kodi tarehe za mwishoni, na wengine kutolipa kodi kwa wakati, hivyo tunaendelea kuwafikia walipakodi kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwasisitiza kulipa kodi kwa wakati ili kuepuka adhabu za kutolipa kodi kwa wakati


Hata hivyo  Meneja TRA ndg Frank Sigareti katika Taarifa yake amesisitiza Taasisi za Umma kudai risiti kwa wakati pindi tuu wanapopewa Huduma na mzabuni, Kwani wazabuni wengi wameonekana kusubiri muda wa malipo ndipo watoe risiti kinyume na sheria,  Risiti inatakiwa itolewe pindi tu huduma inapotolewa au malipo ya huduma yanapofanyika kitakacho anza mapema ndicho kitalazimisha risiti itolewe kwa muda huo huo.


"Wazabuni wanapoomba zabuni kwenye Mfumo wa NEST ni vema Taasisi zetu zikadai Nyaraka muhimu pindi wanapoingia Mkataba na Wazabuni kwa mfano; Tax clearance na Cheti cha usajili wa VAT hii inatusaidia sana katika ukusanyaji wa Kodi


Vile vile Wananchi wanapaswa kuhakikisha wanadai risiti za EFD pindi tuu wanaponunua bidhaa na wafanyabiashara kuacha tabia ya kutotoa risiti halali kwani wakibainika  faini yake ni milioni mbili hadi Milioni nne (2,000,000-4,000,000)


Sambamba na hilo Meneja TRA Wilaya amesema Kodi ya Zuio ya Pango la Biashara anaetakiwa kulipa ni Mwenye Nyumba lakini namna ya kulipa analipa Mfanyabiashara.

Hii ikiwa na maana kuwa Mfanyabiashara anapaswa azuie asilimia 10 ya malipo ya Pango kwa mujibu wa Sheria Ili ailipe TRA.


Mwisho Ndg. Frank Sigareti Meneja TRA Wilaya ya Manyoni amewashukuru sana Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi kwa Ushirikiano mkubwa wanaompatia katika kutimiza majukumu yake ya kukusanya Kodi ya Serikali yeye na Timu yake


"Namshukuru sana Mkurugenzi Manyoni na Mkurugenzi Itigi kwakweli wananipa ushirikiano mzuri sana hata kufanya utendaji wangu wa kazi kuwa rahisi, tuendelee hivyo hivyo Ili kujenga Manyoni yetu kwa pamoja".


###Pamoja Tunajenga Taifa Letu ###

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWAAJILI YA SHUGHULI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 15, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • FOMU YA MAOMBI YA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 12, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA GOTHOMIS NA GePG

    June 25, 2025
  • "LAZIMA TUTANGAZE UTAJIRI TULIONAO MANYONI" DED TUTUBA

    June 25, 2025
  • "LAZIMA TUTANGAZE UTAJIRI TULIONAO MANYONI" DED TUTUBA

    June 25, 2025
  • "UMOJA NI MOJA YA TUNU YA TAIFA LETU HIVYO TUNA JUKUMU LA KUUENDELEZA"

    June 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA MANYONI

    Sanduku la Posta: S.L.P 60 MANYONI

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 26 2540136

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.