• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

Bodi ya TARI yafurahishwa na Kilimo cha Korosho Manyoni

Imewekwa Mtandaoni mnamo: November 19th, 2020

Wakulima wa korosho wilayani Manyoni wametakiwa kuzingatia mafunzo na maelekezo yote wanayopatiwa na watalaamu wa kilimo ili kuweza kuimarisha na kuboresha kilimo cha korosho kuwa bora na chenye tija.

Hayo yamesemwa tarehe 18/11/2020 na BODI ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo nchini (TARI) walipotembelea Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni katika ziara yao ya kuangalia mafanikio ya kilimo cha Korosho ikiwa ni moja ya maagizo yanayotekelezwa na Taasisi hiyo kupitia Taasisi ya Utafiti wa kilimo cha Korosho Naliendele.

Akizungumza kwa nyakati tofauti Mkurugenzi wa Bodi hiyo, Dkt Yohana Budeba ametoa wito kwa watafiti wake sambamba na wadau wa taasisi hiyo kuhakikisha wanaongeza kasi zaidi katika kuleta mapinduzi ya kilimo, aliwataka watafiti na wadau wengine wa kilimo kuunga mkono juhudi za serikali ili kuchagiza kasi ya mabadiliko hayo, sanjari na kusukuma ukuaji wa uchumi. 

“Kwa mujibu wa Rais Magufuli serikali imedhamiria kuongeza juhudi ili kubadilisha kilimo cha Tanzania kuwa cha kibiashara. Hivyo ni jukumu letu watafiti na wakulima kwenda pamoja na dhamiri hiyo njema ili kuongeza tija” alisema Budeba

Alisema katika kuhakikisha inasimamia utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo na maelekezo ya serikali, Bodi yake imefarijika sana kuona utekelezwaji wa maagizo ya bodi hiyo inayoundwa nawajumbe 12 kutoka taasisi na wadau mbalimbali,

Moja ya agizo lilikuwa ni kuitaka TARI kufanya tafiti yenye lengo la kupanua wigo wa kilimo cha zao la korosho kutoka mikoa 5 iliyokuwa ikilima zao hilo, jambo ambalo nalo limetekelezwa ipasavyo kwa taasisi hiyo mpaka sasa kufanikisha kwa tija uanzishwaji  wa kilimo cha zao hilo kwa mikoa takribani 20 ikiwemo Singida, ambayo alipongeza kwa kuendelea kufanya vizuri hususan kupitia shamba lake la Masigati, Manyoni lenye takribani ekari elfu 22 zinazolimwa zao hilo kwa tija na mafanikio makubwa

Dr Budeba pia aliwapongeza mkuu wa wilaya ya Manyoni Mh Rahabu Mwagisa na Mkurugenzi wa halmashauri ya Manyoni ndugu Charles Fussi pamoja na watendaji  wanaosimamia kilimo kwa kuonesha moyo wa kusimamia wakulima na kukubali kulima zao la korosho ambapo kwa msimu wa 2020/2021 wakulima wanatarajiwa kuvuna mazao na kuingia kwenye soko.

Lakini pia amepongeza mkoa wa Singida hususani wilaya ya Manyoni kwa kubuni zao la kimkakati na kuteua baadhi ya maeneo ili kulima korosho

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TARI nchini, Dkt Geofrey Mkamilo, alisema hitaji la Taasisi hiyo kwa sasa ni kuona uzalishaji wa teknolojia zake, ubunifu na mbinu bora za kilimo zinakwenda sambamba na ukuaji wa viwanda-huku taasisi ikiahidi kuongeza juhudi katika kuhakikisha kiwango cha asilimia 60 za malighafi ya kilimo kwenye viwanda vya ndani na zaidi ya hapo inafikiwa ipasavyo.

Alisema pamoja na mambo mengine, shabaha iliyopo mbali ya kupanua wigo wa huduma za kiugani kwa kushirikiana na wadau, taasisi imejipanga kuongeza uzalishaji wa mbegu za korosho ili kukidhi mahitaji ya mikoa yote 20 inayolima zao hilo, na stratejia iliyopo ni kuzalisha kutoka wastani wa tani takribani laki 3 zinazozalishwa kwa sasa kufikia tani milioni 1 ifikapo 2024.

“Maono ya Rais Magufuli ni kuona tija inaongezeka zaidi kupitia hasa mazao haya ya kimkakati likiwemo zao la korosho. Na katika hili tumejipanga vizuri kuhakikisha tunakwenda kuzalisha mabilionea wa kutosha kupitia takribani mazao yote 85 ikiwemo korosho tunayoshughulika nayo, lengo ni kumtoa mkulima kutoka kwenye kilimo cha kujikimu kwenda kwenye kile cha kibiashara” alisema Mkamilo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWAAJILI YA SHUGHULI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 15, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • FOMU YA MAOMBI YA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 12, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBUNI MJIPATIE VIWANJA KWA BEI NAFUU

    May 05, 2025
  • "KIKAO CHA PHC CHAFANYIKA"

    April 26, 2025
  • "Jimbo la Manyoni Mashariki kubadilishwa Jina"

    April 26, 2025
  • "UJUZI UTABADILISHA MAISHA YA WATANZANIA"

    March 23, 2025
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA MANYONI

    Sanduku la Posta: S.L.P 60 MANYONI

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 26 2540136

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.