• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

"DC MANYONI AWATAKA WAZAZI KUHAKIKISHA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA WANARIPOTI SHULE HARAKA IWEZEKANAVYO KATIKA SHULE ZA SEKONDARI WALIZOPANGIWA"

Imewekwa Mtandaoni mnamo: January 18th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Manyoni Mhe. Rahabu Mwagisa ametoa wito huu jana tarehe 17 januari 2023 baada ya kutembelea shule mbalimbali za msingi na sekondari akiambatana na Kamati ya siasa ya Wilaya ilipokua ikifatilia Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), Ameona hali ya mwenendo mahudhurio ya wanafunzi wa kidato cha kwa kwanza kurepoti katika shule walizopangiwa, ambapo hadi sasa idadi ya wanafunzi walioripoti hairidhishi ikilinganisha na matarajio.


“  Wito wangu Nataka wazazi walete wanafunzi kuripoti shule walizopangiwa kidato cha kwanza  haraka iwezekanavyo kwakua Elimu ni bure na huku wakiendelea kukamilisha mahitaji mengine, Walimu wapokeeni wanafunzi hata kama bado hana sare za shule watakamilisha taratibu. Nimepita katika shule chache ambazo tumeona mahudhurio ya wanafunzi kuripoti sio mazuri , nimepita Sasilo, saranda imeonesha hali halisi.

Ifikapo tarehe 30 januari wanafunzi wote wawe wamesharipoti shule walizopangiwa kwa ambao hawataleta wanafunzi hatua kali zitachukuliwa dhidi yao. Watendaji na viongozi wengibne wa serikali naomba mlisimamie hili kuhakikisha watotot wanaripoti shule wote ifikapo tarehe 30 na muwabaini ambao watakua hawajaripoti kwa hatua Zaidi za kisheria”. Amesisitiza Mhe. Mwagisa.




Aidha kutokana na hali hiyo Mhe. Mwagisa  aliwataka wazazi kutambua wajibu wao na umuhimu wa Elimu kwa Watoto, Hivyo basi wahakikishe Watoto wanaripoti shuleni mapema na kwa muda uliopangwa.

 Serikali ya Awamu ya sita chini ya Mhe Dkt Samia Suluhu Hassani Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kutenga fedha kwaajili ya kuboresha miundombinu ya vyumba vya madarasa nchi nzima ili kuleta utoshelevu wa mazingira ya kujifunza na kujisomea kwa idadi ya wanafunzi waliopangiwa katika shule hizo hvyo ni wajibu wetu kuiunga mkono serikali ya awamu ya sita kwa kuhakikisha Watoto wanafika shuleni mapema kwaajili ya kuanza masomo yao.



Sambamba na hilo Mhe. Mwagisa amewataka Wakuu wa Shule kwa kushirikiana na Kamati za Shule kuitisha mikutano ya mara kwa mara na wazazi wa wanafunzi ili kukumbushana wajibu na majukumu katika kutimiza haki za msingi za wanafunzi kupata elimu ikiwa ni pamoja na kutambua kuwa wanafunzi wanapaswa kuripoti shuleni mapema ili kuendana sawa na mihula ya shule na kuhakikisha wanfunzi wanasoma kuanzi siku ya kwanza aliyopaswa kuwepo shuleni.

“Kuna haja ya kuwepo mikutano ya wazazi ya mara kwa mara katika shule zetu hivyo niwaombe sana walimu mkishirikiana na kamati zenu za Shule kuandaa mikutano hii na kukumbushana juu ya wajibu wa  mzazi na jamii inayomzunguka kwa ujumla  ili kuhakikisha wanafunzi hawa wanapata elimu kikamilifu na kwa wakati sahihi, Moja ya wajibu wa wazazi kwa  wanafunzi ni pamoja na kuhakikisha wanafunzi wanaripoti shuleni siku ya kwanza wanapofungua shule ili waende sawa na muhula ulivyopangwa”

“Nitoe wito kwa Walimu kutoa elimu kwa wazazi kuhusu umuhimu wa elimu pamoja na malezi kwa Watoto kutokana na wazazi wengi kupuuzi umuhimu wa elimu kwasasa na kupelekea kuathiri mwenendo w a wanfunzi katika ufaulu. Pia amewaomba walimu kutoa elimu ya malezi kwa kushirikiana na wazazi kwasababu wanafunzi wengi kwa sasa wana changamoto ya malezi hali inayopelekea mporomoko mkubwa wa maadili na kuathiri ufaulu wa wanafunzi”



 

Ni Imani yangu kuwa viongozi mnakwenda kuyasimamia haya niliyoyasema hapa na kuhakikisha ifikapo tarehe 30 januari wanafunzi wote ambao ni matarajio yetu kwa mwaka 2023 wanaripoti shuleni kwa shule zote kwa kidato cha kwanza na darasa la kwanza na Awali. Serikali imeweka mpango bora wa elimu bure ili kuhakikisha Watoto wote wa jinsia zote wanapata elimu bora na kwa usawa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWAAJILI YA SHUGHULI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 15, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • FOMU YA MAOMBI YA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 12, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBUNI MJIPATIE VIWANJA KWA BEI NAFUU

    May 05, 2025
  • "KIKAO CHA PHC CHAFANYIKA"

    April 26, 2025
  • "Jimbo la Manyoni Mashariki kubadilishwa Jina"

    April 26, 2025
  • "UJUZI UTABADILISHA MAISHA YA WATANZANIA"

    March 23, 2025
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA MANYONI

    Sanduku la Posta: S.L.P 60 MANYONI

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 26 2540136

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.