• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

Manyoni Yaendelea Kusimamia Afua za Lishe, Afya ya Mama na Mtoto Kupitia Kikao Kazi cha Tathmini ya Utekelezaji

Imewekwa Mtandaoni mnamo: August 22nd, 2025

Manyoni Yaendelea Kusimamia Afua za Lishe, Afya ya Mama na Mtoto Kupitia Kikao Kazi cha Tathmini ya Utekelezaji


Manyoni, 21 Agosti 2025 – Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni imeendesha kikao kazi muhimu cha kujadili utekelezaji wa mkataba wa lishe, tamko la “Jiongeze Tuwavushe Salama”, pamoja na maendeleo ya Mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa (iCHF).


Kikao hicho kilichoongozwa na Katibu Tawala wa Wilaya, Mwalimu James Mchembe, kilihudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka idara za afya, mipango, ustawi wa jamii, elimu na mashirika yanayoshiriki katika kuboresha afya ya jamii. Katibu wa kikao alikuwa Afisa Mipango na Uratibu, Bi. Mery Kanumba.


Katika kikao hicho, ajenda kuu zilijikita katika:

- Tathmini ya Mkataba wa Lishe ngazi ya halmashauri.


- Utekelezaji wa Tamko la “Jiongeze Tuwavushe Salama” linalolenga kuboresha afya ya mama mjamzito, uzazi salama na malezi ya watoto wachanga;

- Uhamasishaji na maendeleo ya Bima ya Afya iliyoboreshwa (iCHF) ikiwa ni mkakati wa kuongeza upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi;

-Taarifa ya utekelezaji wa programu ya M-MAM kwa kipindi husika.


Mwenyekiti wa kikao, Mwalimu Mchembe, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya idara na sekta mbalimbali katika kutekeleza afua za afya, lishe, na ustawi wa jamii. Alihimiza pia ukusanyaji sahihi wa takwimu na ufuatiliaji wa karibu wa viashiria vya mafanikio katika maeneo yote ya utekelezaji.


Bi. Mery Kanumba, kwa upande wake, alieleza kuwa halmashauri inaendelea kuimarisha mikakati ya utekelezaji kwa kushirikisha jamii, viongozi wa vijiji na wadau wa maendeleo ili kuhakikisha watoto, akina mama, na familia kwa ujumla wananufaika na afua hizi, Pia aliwataka Maafisa kuwaelimisha Wazazi ili wapate uelewa juu ya umhimu wa lishe mashuleni na kupinga ndoa za utotoni.


Washiriki wa kikao walijadiliana kwa kina changamoto, mafanikio na mikakati ya kuboresha utekelezaji wa afua hizo katika robo inayofuata, huku wakiahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu kuhakikisha jamii ya Manyoni inanufaika na huduma bora za afya na lishe.


@ortamisemi

@singidars

@halimadendego

@drmashinjivincent

@anastaziatutuba

@manyonidcfootball

@wizara_afyatz

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWAAJILI YA SHUGHULI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 15, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • FOMU YA MAOMBI YA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 12, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani Yang’ara Solya Sekondari

    October 11, 2025
  • Wananchi Kintinku, Maweni na Makanda Wapewa Elimu ya Umiliki wa Ardhi – “Tuwe na Hati Miliki” Asema Afisa Ardhi

    October 09, 2025
  • Kamati ya Ushauri wa Kisheria Yatoa Msaada Manyoni: “Tuko Hapa Kwa Ajili ya Haki Zenu

    October 09, 2025
  • TANGAZO MAALUM LA WANANCHI

    October 07, 2025
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA MANYONI

    Sanduku la Posta: S.L.P 60 MANYONI

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 26 2540136

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.