• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

Nape Amshukuru Rais Samia Kuipa Nguvu Kamati ya Kutathmini Uchumi Vyombo vya Habari

Imewekwa Mtandaoni mnamo: May 24th, 2023



Na Lilian Lundo - MAELEZO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kuipa nguvu Kamati ya Kutathmini Hali ya Uchumi wa Vyombo vya Habari, baada ya kutoa maelekezo wakati wa hafla ya uzinduzi wa minara ya kurusha matangazo kwa masafa ya ardhini (DTT) kuwa kamati hiyo isifanye haraka kutoa taarifa bali ifanye utafiti wa kina na kutoa taarifa iliyokamilika.


Shukrani hizo zimetolewa leo Mei 23, 2023 na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye wakati akipokea taarifa ya utekelezaji wa kamati hiyo ambayo aliiunda Januari 24, 2023.


"Serikali inategemea sana matokeo ya kazi itakayofanywa na kamati hii, katika kutengeneza mifumo itakayobadilisha tasnia ya habari. Tasnia ya habari na changamoto zake haziwezi kumalizwa na matamko ya kisiasa, zitamalizwa kwa kutengenezwa mifumo ambayo inatengenezwa kwa tafiti pamoja na kuhusisha mawazo ya watu wengi," amesema  Nape.


Ameendelea kusema kuwa, mwanzoni alitoa miezi mitatu akidhani kazi itakuwa ndogo, lakini kazi imekuwa kubwa na kwa ramani waliochora wataalam hata miezi Sita  iliyoomba kuongezewa na kamati  inaweza ikawa ni michache.


"Baada ya kupata ripoti nimekubaliana nao, tuwape hiyo miezi sita, badala ya ile mitatu ya mwanzo, ili wakamilishe hii kazi ambayo wameshaianza. Wito wangu kwa Wanahabari na Wadau wa Habari ni kutoa ushirikiano kwa kamati ili wakamilishe kazi, na hatimaye kazi ya Uandishi wa Habari iwe na heshima inayostahili," amesema Nape.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Tido Mhando amesema kuwa, baada ya kuwahusisha wataalam wa masuala ya utafiti wa masuala ya habari na uchumi, kamati iliona inahitaji muda zaidi wa kufanya utafiti huo.


"Suala zima la uchumi haliishii tu kwenye mishahara ya wafanyakazi lakini vilevile mambo mengine mengi, mfano namna gani vyombo vya habari vinaweza kuboresha na kupata mafanikio yanayostahili," amesema Tido.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWAAJILI YA SHUGHULI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 15, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • FOMU YA MAOMBI YA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 12, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBUNI MJIPATIE VIWANJA KWA BEI NAFUU

    May 05, 2025
  • "KIKAO CHA PHC CHAFANYIKA"

    April 26, 2025
  • "Jimbo la Manyoni Mashariki kubadilishwa Jina"

    April 26, 2025
  • "UJUZI UTABADILISHA MAISHA YA WATANZANIA"

    March 23, 2025
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA MANYONI

    Sanduku la Posta: S.L.P 60 MANYONI

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 26 2540136

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.