• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Imewekwa Mtandaoni mnamo: March 10th, 2022

Katika kusherehekea siku ya wanawake Duniani wilayani Manyoni wanawake wametakiwa kutambua kuwa wao wanajukumu kubwa sana katika Taifa hili katika kutimiza wajibu wao  kusimamia haki zao pamoja na makuzi ya watoto na kupinga ukatili wa kijinsia kwa watoto na wanawake.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Rahabu Mwagisa wakati  akihutubia katika sherehe za maadhimisho hayo yaliyofanyika katika kata ya saranda wilayani Manyoni

Mwagisa amesema kuwa  kila ifikapo march 8 duniani kote wanaadhimisha siku ya wanawake lengo ikiwa ni kuweza kuwakumbusha wanawake majukumu yao katika malezi na makuzi ya watoto lakini pia kuikumbusha jamiikutambua umuhimu wa mwanamke katika jamii , kuwasaidia wanawake kuweza kutambua haki zao  na za watoto ambapo amewataka wanawake kuacha kusherehekea siku hiyo kwa mazoea bali wasimamie kauli mbiu na kuhakikisha wanaitekeleza na kuifanyia kazi kwa kutimiza majukumu yao.

Mwagisa aliongeza kuwa  wajibu wa kila mwanamke ni  kulinda haki na usawa kwa watoto na wanawake, nakuwataka wanawake kujua kuwa jukumu kubwa la kulea watoto ni la wanawake hivyo amewataka kuacha kujisahu kutimiza majukumu yao na badala yake wajitambue na kujua kuwa mtoto yeyote anapoharibikiwa mzigo huwa kwa mama yake

“mtoto mwenye hekima humfurahisha babaye bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamae maandiko yanasema pia, hivyo wanawake wenzangu tusijisahau tuhakikishe tunasimamia malezi ya watoto wetu huko majumbani na hata mitaani tujue kuwa mtoto wa mwenzio ni mtoto wako pia lakini   ndugu zangu tusisherehekee tu kama mazoea bali tujue tunajukumu kubwa kama nguzo ya Taifa tusijisahau sisi wanawake, sambamba na kutia nguvu kauli mbiu yetu tuendelee kupambana na vitendo viovu vinavyojitokeza kwa wanawake na watoto”alisema Mwagisa

Mwagisa alipata fursa ya kuwapongeza walimu na kuwaomba waendelea kuwa chachu ya malezi na kupambana na vitendo viovu juu ya usimamizi na makuzi ya mtoto.

“kwa nini ninasema walimu, niaamini mnamchango mkubwa sana kama wanawake katika Taifa hili kwani nyie mnakaa na watoto wetu kwa masaa mengi hivyo ninaimani kuwa mnamchango mkubwa sana wa malezi zidi ya watoto wetu, niwaombe sana walimu tukumbushanena tusimamie malezi ya watoto wetu tutambuwe kuwa msichana wa leo ndiyo mwanamke wa kesho hivyo niwaombe sana tuwalinde mabinti zetu.”alisisitiza Mwagisa

Katika suala la maendeleo na kujikwamua kiuchumi Mwagisa aliwataka wanawake wa Wilaya ya Manyoni kutumia fursa mbalimbali zinazopatikana katika Halmashauri lakini pia kushirikiana na ofisi ya Maendeleo ya jamii ya Wilaya kuweza kuibua vyanzo mbalimbali vya mapato ili kuweza kujikwamua kiuchumi na kuongeza kipato ili waweze kusimamia familia zao.

“ wanawake tukijikwamua kiuchumi tutaweza kusaidia wenza wetu kwani kwa kufanya hivyo tutapunguza kasi ya umaskini lakini pia itatujengea heshima tutaweza kujisimamia hivyo basi niwaombe  tutumie mikopo mbalimbali na pia tufanyeshughuli mbalimbali  ili tuweze kuleta tija ya maendeleo ya jamii yetu”aliongeza Mwagisa

Aidha Mwagisa amempongeza Mh Rais mama Samia Suluhu Hassan kwa kutoa bilioni 6 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika Halmashauri ya Manyoni  amewaomba wamama kuweza kumuunga Mh Rais  Samia Suluhu Hassan mkono katika kusimamia majukumu yote kama wanawake .

Awali akisoma taarifa ya maadhimisho hayo afisa maendeleo msaidizi Ostatila Mwilafi amesema kuwa lengo la maadhimisho hayo ni kumuuonyesha upendo ,mwanamke kutokana na mafanikio yake katika Nyanja mbalimbali kama vile siasa kijamii na kiuchumi, ni siku ambayo wanawake hutambuliwa kutokana namafanikio yao bila kujali mgawanyiko wa Taifa bila kujali kabila lugha itikadi utamaduni kiuchumi au kisiasa

Aidha amesema kuwa nchini Tanzania maadhimisho haya hufanyika ilikutathmini maendeleo ya mwanamke  kuwakumbusha wadau na jamii kuhusu umuhimu wa wanawake katika kuchangia ujenzi wa Taifa aidha wanawake ni kitovu cha mabadiliko chanya katika jamii.

Mwilafi alisema Halmashauri ya Manyoni wanawake wamekuwa wakishirikishwa katika Ngazi  zote hasa katika masuala ya kusimamia na kutekeleza mipango ya kimaendeleo aidha wanawake wamejengewa uwezo kupitia mafunzo mbalimbali yanayotolewa na wadau na Halmashauri pia wamewezeshwa kiuchumi kupitia mikopo nafuu.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii Frola Hindi amewataka wanawake kujikomboa kimaisha ili kuweza kutimiza majukumu ya familia amewataka  kubadilika na kuzingatia masuala ya kimaendeleo lakini pia amewataka wanawake kuwa na ujasili na kwamba pale wanapofanyiwa ukatili basi kuchukua hatua kufika katika vyombo husika vinavyojihusisha na kusimamia haki za mwanamke.

Akihitimisha sherehe hizo Mh Mariamu  Palingo Diwani wa viti maalumu Tarafa ya Saranda amesema kuwa anawashukuru watu wote kwa ushrikiano wao katika maadhimisho hayo lakini pia amewaagiza wanawake kutekeleza yale yote yaliyoagizwa na kuhakiksha wanasimamia kwa ukamilifu ili kupata kizazi chema na chenye uadilifu.

Aidha atika sherehe hizo baadhi ya wadau washiriki kama vile NMB,CRDB,MAHAKAMA,USTAWI WA JAMII,CAMFED na Wadau wengine waliweza kutoa taarifa zao ,na shirika la Cama Member Association kwa kushirikiana na CAMFED waliweza kutoa zawadi za madaftari na kalamu kwa wanafunzi wa shule za saranda zawadi zenye thaman ya tsh 70,000/=.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWAAJILI YA SHUGHULI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 15, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • FOMU YA MAOMBI YA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 12, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBUNI MJIPATIE VIWANJA KWA BEI NAFUU

    May 05, 2025
  • "KIKAO CHA PHC CHAFANYIKA"

    April 26, 2025
  • "Jimbo la Manyoni Mashariki kubadilishwa Jina"

    April 26, 2025
  • "UJUZI UTABADILISHA MAISHA YA WATANZANIA"

    March 23, 2025
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA MANYONI

    Sanduku la Posta: S.L.P 60 MANYONI

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 26 2540136

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.