• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

“UTAMBUZI WA ENEO LA UJENZI WA VETA KINTINKU-LUSILILE KATIKA WILAYA YA MANYONI "

Imewekwa Mtandaoni mnamo: March 24th, 2023

Tarehe 23 machi 2023 Timu kutoka Ofisi ya Uthibiti Ubora wa Shule Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni imetembelea Kijiji cha Lusilile kilichopo kata ya Kintinku Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kutambua Eneo ambalo litatumika kujenga Chuo cha VETA ikiwa ni Miongoni mwa Vyuo  63 vitakavyojengwa Nchini Tanzania.

 

Kaimu Mthibiti Mkuu Ubora wa Shule Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni  Ndg.Peter Noel Foya ambaye pia ndiye  amepewa madaraka ya kusimamia mradi na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia (WYEST) aliwajulisha viongozi wa Kijiji cha lusilile kuwa lengo la Ziara yake ni kutambua eneo la utekelezaji wa mradi wa kujenga chuo cha VETA pamoja na kutambua mipaka.

“Leo nimekuja na Timu yangu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Ofisi ya Uthibiti Ubora wa Shule ili kuona eneo mlilolitenga kwaajili ya kujenga Chuo cha VETA na kutambua zUkubwa wake pamoja na Mipaka ya eneo hili”

Ndg Foya alisema, Mradi huu wa Ujenzi wa Chuo cha VETA  utakuwa awamu mbili (2)ambapo awamu ya kwanza zimetolewa kiasi cha Tsh. Bilioni 1.4 ili kuanza kujenga  Miundombinu ya majengo 9 ambayo ni : Jengo moja la utawala, jengo moja la darasa, kibanda kimoja cha mlinzi, nyumba moja ya Mkuu wa Chuo,jengo la karakana tatu(3), jengo moja la choo na jengo moja la umeme.

 Kwa ngazi ya taifa vitakuwa vyuo 64 ambapo vyuo 63 vitakuwa katika ngazi ya wilaya na chuo kimoja(1) ngazi ya mkoa ambapo kitajengwa katika mkoa wa SONGWE na kwa SINGIDA wilaya zilipatiwa mradi ni Manyoni, Iramba na Mkalama hivyo kipekee Tunamshukuru Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassani kwa kutupatia mradi huu katika Wilaya ya Manyoni.Alisisitiza Ndg Foya.


Ndg Foya amesema, Mradi utatekelezwa kwa kutumia FORCE AKAUNTI na kuanzia tarehe 27/3/2023 matangazo ya zabuni yatakuwa yametoka pamoja na taratibu za manunuzi na Ujenzi utaanza mwezi APRIL hadi SEPTEMBER 2023.

 Mshauri mwelekezi wa mradi ambaye ameteuliwa na wizara ya elimu kwa utekelezaji wa mradi wa wilaya ya Manyoni atatoka BICO( Bureau of Industrial Cooperation) kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam hivyo niwaombe kutoa ushirikiano wa Kutosha pindi tutakapoanza Mradi wa Ujenzi wa Chuo hiki cha VETA katika Wilaya yetu ya Manyoni.alisisitiza Ndg Foya.


Naye Afisa tarafa ya Kintinku Ndg. Charles Andrew Magesa amesema,Ninaishukuru sana Serikali ya Awamu ya sita chini ya Raisi wake Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassani kwa kutupati amradi huu katika Wilaya ya Manyoni na cha zaidi nashukuru kwakua mradi huu unakwenda kutekelezwa ndani ya tarafa yangu ya Kintinku ,Tunashukuru kwa kupatiwa mradi mkubwa na wenye tija kwa vizazi vijavyo.

 Ndg Magesa alisema, Kijiji hiki cha Lusilile kata ya Kintinku kimetenga hekari 48.7 kwaajili ya Mradi huu na niwaombe tulitembelee eneo hili ili kujirizisha na kuona Mipaka.

Sambamba na Kutembelea Eneo hilo na kuliona na kutambua mipaka Ndg Elizabeth Edward Mchele mwakilishi wa Afisa Ardhi wa Wilaya ya Manyoni ameweka alama kwenye eneo hilo la ujenzi  na kuwahidi kuwa Maafisa Ardhi Wilaya ya Manyoni watakuja kuchukua vipimo halisi vya eneo siku chache zijazo kabla ya ujenzi wa mradi kuanza.

Katika ziara hiyo ya Utambuzi wa Eneo la Ujenzi wa Mradi  viongozi mbalimbali walishiriki  HUSSEINI KAlESO-  Mwenyekiti wa Kijiji lusilile, HALIMA SEIF- VEO Kijiji cha lusilile, MAGRETH MASAMI- WEO kata ya kintinku,IMANI SAMWEL LECHIPYA-Mhasibu wa Idara ya Uthibiti Ubora wa Shule,RAYMOND ERICK MWASHALAWE-Afisa Ugavi Idara ya Uthibiti Ubora,ALBERT CHILUMATE- Mwenyekiti wa Bodi ndogo ya zabuni.


Imetolewa na;

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Halmashauri ya Manyoni.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWAAJILI YA SHUGHULI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 15, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • FOMU YA MAOMBI YA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 12, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBUNI MJIPATIE VIWANJA KWA BEI NAFUU

    May 05, 2025
  • "KIKAO CHA PHC CHAFANYIKA"

    April 26, 2025
  • "Jimbo la Manyoni Mashariki kubadilishwa Jina"

    April 26, 2025
  • "UJUZI UTABADILISHA MAISHA YA WATANZANIA"

    March 23, 2025
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA MANYONI

    Sanduku la Posta: S.L.P 60 MANYONI

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 26 2540136

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.