• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

WALIMU WA HISABATI SHULE ZA MSINGI MANYONI WAPEWA MAFUNZO KUINUA UFAULU

Imewekwa Mtandaoni mnamo: September 19th, 2025

*WALIMU WA HISABATI SHULE ZA MSINGI MANYONI WAPEWA MAFUNZO KUINUA UFAULU*

*Manyoni, 19 Septemba 2025*


Mradi wa Serikali wa Shule Bora unaofadhiliwa na UKAID wenye lengo la kukuza na kuboresha Ufundishaji na ujifunzaji umeendesha mafunzo ya siku tatu kwa Walimu wa somo la Hisabati kutoka shule za msingi zote ndani ya halmashauri ya Manyoni, kwa lengo la kuboresha ufundishaji na ujifunzaji wa somo hilo muhimu.


Mafunzo hayo yalianza tarehe 17 na kukamilika leo tarehe 19 Septemba 2025, yakifanyika katika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni yakihusisha wakufunzi wenye uzoefu kutoka Idara ya elimu Mkoa,Wilaya pamoja Wasimamizi wa Mradi huu kutoka Shirika linalofadhili mradi.


Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo, Mary Kanumba Kaimu Mkurugenzi Halmashauri wilaya ya Manyoni alieleza kuwa Hisabati ni somo la msingi katika maendeleo ya kielimu, lakini limekuwa likiwa changamoto kwa baadhi ya wanafunzi. Hivyo, kupitia mafunzo haya, walimu watapewa mbinu shirikishi, rahisi na bunifu zitakazowasaidia wanafunzi kuelewa kwa urahisi.


*"Tunatarajia kila mwalimu atakaporudi katika shule yake, atakuwa na mkakati mahsusi wa kuongeza ufaulu katika somo la Hisabati. Hatutarajii kuona wanafunzi wanaogopa au kushindwa somo hili tena,"* alisema Mary Kanumba


Walimu walioshiriki walisema watajifunza mbinu mpya za kufundisha dhana ngumu za Hisabati, kutumia vifaa saidizi, pamoja na namna ya kufanya tathmini ya maendeleo ya mwanafunzi mmoja mmoja.


Mafunzo haya ni sehemu ya mkakati wa Halmashauri ya Manyoni kuinua kiwango cha ufaulu wa masomo ya msingi, hasa Hisabati, kama msingi wa mafanikio ya elimu ya juu.

@wizara_elimutanzania

@maelezonews

@singidars

@shulebora_programme

@drmashinjivincent

@anastaziatutuba

@ortamisemi

@msemajimkuuwaserikali

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWAAJILI YA SHUGHULI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 15, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • FOMU YA MAOMBI YA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 12, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani Yang’ara Solya Sekondari

    October 11, 2025
  • Wananchi Kintinku, Maweni na Makanda Wapewa Elimu ya Umiliki wa Ardhi – “Tuwe na Hati Miliki” Asema Afisa Ardhi

    October 09, 2025
  • Kamati ya Ushauri wa Kisheria Yatoa Msaada Manyoni: “Tuko Hapa Kwa Ajili ya Haki Zenu

    October 09, 2025
  • TANGAZO MAALUM LA WANANCHI

    October 07, 2025
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA MANYONI

    Sanduku la Posta: S.L.P 60 MANYONI

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 26 2540136

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.