• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akagua ujenzi wa miradi ya maji katika Halmashauri ya Manyoni.

Imewekwa Mtandaoni mnamo: February 13th, 2019

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mh. Prof Makame Mbarawa ametembelea miradi mbalimbali ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni ambapo aliambatana na mwakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni ndugu Chales Edward Fussi pamoja na Mbunge wa Manyoni Mashariki Mh. Daniel Mtuka.

Miongoni mwa miradi iliyotembelewa na Mh Waziri ni Chanzo cha Mradi wa maji wa Kintinku/Lusilile katika Kijiji Cha Mbwasa Kata ya Makutupora, Tarafa ya Kintinku Wilayani Manyoni ambapo pia alipata muda wa kuzungumza na viongozi mbalimbali wakiwemo wakuu wa idara na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni.

Waziri wa Maji, Mhe. Profesa Makame Mbarawa amewataka wahandisi wote nchini kusimamia wakandarasi wanaojenga miradi ya maji kikamilifu na kwa uadilifu. Hayo aliyasema alipokuwa akikagua miradi ya maji inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni ambayo kwa sasa kuna ujenzi wa mradi wa maji wa Kintinku/Lusilile awamu ya kwanza ukiwa unatekelezwa.

Mradi huu wa maji wa Kintinku/Lusilile ni mradi mkubwa ambao ukikamilika utahudumia takribani wakazi 55,485 wanaoishi katika vijiji 11. Mradi huu unategemea kugharimu kiasi cha takribani Tshs. 10,171,877,293.05.

Aidha, Mhe. Waziri amemsifu sana mkandarasi anayetekeleza mradi huu M/S CMG Construction Company ambaye ameanza utekelezaji wa ujenzi na ameshawasilisha “certificate” zake lakini bado hajalipwa. 

Waziri amemuagiza Mhandisi wa Wilaya kuzihakiki “certificate” hizo za malipo ya mkandarasi huyo na kuzipeleka kwenye ngazi ya mkoani ili nako zihakikiwe ili mkandarasi huyo aweze kulipwa.

“Nitamlipa mkandarasi mwezi huu wa Februari, lakini naomba kutoa angalizo mkoa mfanye uhakiki wa kina kabla ya kuzileta Wizarani na msipofanya uhakiki wa kina nitazirejesha”, alisema Waziri Mbarawa.

Naye Mbunge wa Manyoni Mhe. Daniel Mtuka alimweleza Waziri Mbarawa kuhusu uanzishwaji wa Mamlaka ya Maji Mauwa, “Manyoni Urban Water Authority” Waziri Mbarawa amesema hana pingamizi. Wapeleke majina atayapitisha ila wachagueni watu  wenye uwezo na siyo mchague watu kwa sababu ya urafiki au undugu. Chagueni watu wazuri watakaoweza kuwasaidia na kufanya kazi ya kusimamia huduma za maji hapa Manyoni.

Kabla ya kumaliza ziara yake Waziri ameeleza kuchukizwa kwake na utendaji kazi mbovu wa Wakala wa Uchimbaji Visima na Ujenzi wa Mabwawa (DDCA) baada ya  Mhe. Mbunge wa Manyoni Bw. Daniel Mtuka kutoa malalamiko kuhusu DDCA kushindwa kukamilisha uchimbaji wa kisima katika Halmashauri ya wilaya ya manyoni. Waziri ameagiza DDCA kukamilisha kazi hizo za kuchimba visima haraka iwezekanavyo na kusisitiza wabadilike ikiwemo mtendaji mkuu kufika na kuona namna ya kasi ya Uchimbaji inavyokwenda

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWAAJILI YA SHUGHULI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 15, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • FOMU YA MAOMBI YA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 12, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBUNI MJIPATIE VIWANJA KWA BEI NAFUU

    May 05, 2025
  • "KIKAO CHA PHC CHAFANYIKA"

    April 26, 2025
  • "Jimbo la Manyoni Mashariki kubadilishwa Jina"

    April 26, 2025
  • "UJUZI UTABADILISHA MAISHA YA WATANZANIA"

    March 23, 2025
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA MANYONI

    Sanduku la Posta: S.L.P 60 MANYONI

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 26 2540136

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.