• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara Kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Manyoni District Council
Manyoni District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • History
        • Orodha Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Mchoro wa Kiutawala
      • Picha Ya Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala & Utumishi
        • Majukumu ya Idara
        • Legal Seatings on Council's level
        • Department Information
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala wa Mazingira na Usafi
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
      • Huduma Zetu
        • Afya
        • Elimu
        • Maji
        • Kilimo
        • Mifugo
        • Uvuvi
    • Kilimo cha Korosho
    • Msimu wa mashamba ya Korosho 2019/2020
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba Ya Picha
    • Matokeo ya Kidato cha Pili 2018

“ZINGATIENI DOZI ZA CHANJO KWA WATOTO” DC MANYONI

Imewekwa Mtandaoni mnamo: April 29th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Kemirembe Lwota amewataka kina mama na wanachi wa manyoni kwa ujumla kuzingatia dozi za chanjo kwa watoto kama inavyokua ikielekezwa na wataalamu wa Afya kwani kutokufata dozi za chanjo kunafanya dawa hizo zisifanye kazi vizuri.

Mhe. Kemirembe ameyasema haya alipokua akizindua maadhimisho ya  wiki ya chanjo kiwilaya jana tarehe 28 aprili 2023 yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya kata ya Muhalala Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni.


                                 

“Nitoe rai kwa kinamama na wananchi wote wa Manyoni; Kuna chanjo huwa zinatolewa zaidi ya mara moja kwa maana kuwa ili dozi yake  ikamilike lazima mtoto apate chanjo zaidi ya mara moja hivyo niwaombe kina mama na wananchi wa Manyoni kwa ujumla  kuhakikisha watoto  wanapata chanjo kikamilifu kwa kufuata na kuzingatia dozi hizi, Sio mtoto anatakiwa kupata chanjo mara nne wewe unapata ya kwanza, ya pili unaruka unampeleka ya tatu huo sio utaratibu naomba mfate dozi ya chanjo kama wataalamu wanavyowaelekeza”


Mhe. Kemirembe amesema; Tunamshukuru Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa kuboresha huduma ya Afya kwetu na kuhakikisha tunapata chanjo hizi bure kwa maana kuwa tayari amelipia dawa hizi za chanjo ndio maana sisi wananchi hatutoi garama yoyote ili kuhudumiwa chanjo hizi, Hivyo tuhakikishe watoto wote wenye umri stahiki wanapata chanjo hizi ili kuwakinga na magonjwa mbalimbali kwani kwa watoto kuwa wazima wakati wote wazazi tunapata Muda mzuri wa kufanya shughuli za kiuchumi lakini wakiwa wagonjwa tutakosa muda wa kukuza uchumi wetu na Taifa kwa ujumla.


Nichukue fursa hii kuwapongeza na kuwashukuru watoa huduma wetu wa Afya kwa jitihada zao kubwa za kuhakikisha chanjo zinawafikia popote wananchi walipo, chanjo zote za magojwa mbalimbali zinatolewa kama vile chanjo ya Rubela, Polio, surua na zinginezo lakini pia kwa kuhakikisha Afya za wananchi wa Manyoni zinakua vizuri wakati wote, Niombe sasa chanjo hizi walau zitolewe mara mbili kwa mwezi ili kuboresha na kuongeza ufanisi zaidi katika kuhakikisha watoto wote wanapata chanjo katika Wilaya yetu ya Manyoni. Alisema Mhe. Kemirembe.


Pia niwashukuru wadau wa Maendeleo ya Afya hasa  CHAI waliofadhili huduma za chanjo katika halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, na wadau wengine wa Afya kama JSI na Mkapa Foundationi wanaotufadhili kifedha lakini pia kitaalamu katika Mkoa wetu na kuongeza muitikio wa waanchi katiaka kupata huduma za Afya na kuimarisha jamii yetu, Aidha napenda kuwafahamisha kuwa Wataalamu wetu wamejipanga vizuri sio tuu kutoa chanjo lakini kutoa huduma zingine za Afya ikiwa pamoja na kutoa elimu ya afya juu ya umuhimu wa kumaliza chanjo, uchangiaji wa damu salama, Afya ya uzazi ,Lishe na Magonjwa yasiyoambikizwa , Magonjwa ya mlipuko na Mengineyo. Alisisitiza Mhe. Kemirembe.


 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWAAJILI YA SHUGHULI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA September 15, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • FOMU YA MAOMBI YA MASHAMBA YA KOROSHO MWAKA 2022/2023 July 04, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 12, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBUNI MJIPATIE VIWANJA KWA BEI NAFUU

    May 05, 2025
  • "KIKAO CHA PHC CHAFANYIKA"

    April 26, 2025
  • "Jimbo la Manyoni Mashariki kubadilishwa Jina"

    April 26, 2025
  • "UJUZI UTABADILISHA MAISHA YA WATANZANIA"

    March 23, 2025
  • Angalia zote

Video

Ngoma za asili Siku ya UKIMWI Duniani
video zingine

Kurasa za Karibu

  • About Manyoni
  • Completed Projects
  • Ongoing Projects
  • Primary Schools Students Registration (Prem)
  • Instagram

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • President's Office, Public Service Management
  • Singida Region
  • Necta
  • MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
  • Kupata Salary Slip

Fuatiliaji ya watembezi wa Kidunia

world map hits counter

Kihesabia Watembezi

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA MANYONI

    Sanduku la Posta: S.L.P 60 MANYONI

    Simu: +255 26 2540136

    Namba ya Simu: +255 26 2540136

    Barua Pepe za Watumishi: ded.manyonidc@singida.go.tz, ded@manyonidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za Siri
    • Malalamiko
    • Maswali ya Mara Kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki Ya Kunakiri ©2019 Halmashauri Ya Wilaya Ya Manyoni . Haki Zote Zimehifadhiwa.